Powered By Blogger
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SHERIA. Onyesha machapisho yote
Inaonyesha machapisho yaliyo na lebo SHERIA. Onyesha machapisho yote

Alhamisi, 8 Februari 2024

Teknolojia Itumike Kutatua Changamoto Ya Ajira Afrika

 

Teknolojia Itumike Kutatua Changamoto Ya Ajira Afrika


Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania, Dkt. Phillip Mpango akizungumza na wadau mbali mbali wa ajira wakati akifungua mkutano wa saba wa washirika wa Kijamii wa Afrika ( ASP). Mkutano huo uulioandaliwa na Chama cha waajiri Tanzania ( ATE) umeanza leo Februari 7,2024 katika ukumbi wa JNICC jijini Dar es Salaam na unatarajiwa kumalizika kesho Februari 8,2024

Na Karama Kenyunko Michuzi Tv
MAKAMU wa Rais Dkt. Phillip Mpango amezitaka nchi za Afrika kuchukua hatua za kutumia maendeleo ya teknolojia ili kukabiliana na ukosefu wa ajira pamoja na ka kuchochea uzalishaji na ukuaji wa uchumi barani humo.

Dkt.Mpango ametoa wito huo leo, Frebuari 6, 2024, wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa 7 wa Washirika wa Kijamii wa Afrika, uliofanyika jijini Dar es Salaam ambapo amewashauri wajumbe wa mkutano kuitazama teknolojia ya akili bandia (AI) kama fursa na kwamba wasihofie.

"Katika eneo la maendeleo ya teknolojia, kunadhaniwa kwamba nafasi za ajira zitaathiriwa na AI. Pamoja na kuwa na dhana hiyo lakini teknolojia hiyo itatengeneza ajira mpya hasa zile zinazohitaji ujuzi wa kiufundi,” amesema

Katika mkutano huo uliohudhuriwa na wajumbe kutoka nchi 50 barani Afrika DKt. Mpango amesema kuwa muhimu kuendeshwe mafunzo yatakayoendana na mabadiliko ya teknolojia na kubaini sekta zenye fursa nyingi za ajira.

"Sekta ambazo akili bandia zinaweza kuongeza ajira ni kilimo ambapo AI inaweza kukuza utafiti wa kilimo kwa kubaini aina ya mbegu bora itakayomudu mabadiliko ya hali ya hewa " alisema.


Akizungumza nje Mkutano huo , Ofisa Mtendaji Mkuu wa Chama cha Waajiri Tanzania (ATE), Suzan Ndomba amesema mkutano huo utajikita katika masuala ya uzalishaji wa ajira kwa mada tofauti na kuja na mapendekezo.

Kwa upande wake, Roberto Suarez Santos, Katibu Mkuu wa Shirika la Kimataifa la Waajiri (IOE) ameema, mkutano huo unatoa fursa ya kuunda suluhisho na mbinu za pamoja za kutatua changamoto za ajira kwa vijana na kwa ukosefu wa utulivu wa kijamii.

Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), Said Wamba, amesema wakiwa wadau shirika lao linatarajia kujadili namna ya kuendeleza mijadala na midahalo yenye nia ya kuboresha uhusiano kati ya chama na waajiri kwa sababu ajira inamnufaisha kila mtu akiwemo mustakabali wa sekta ya ajira.

DKT. SAMIA ASISITIZA UCHAGUZI UTAKUWA WA DEMOKRASIA, WA HAKI, SHERIA NA UTAWALA BORA.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema haki, demokrasia, sheria na utawala bora utadumishwa kwa watu wote wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu.


Rais Samia amesema hayo leo katika sherehe za mwaka mpya 2024 (Diplomatic Sherry Party) kwa Mabalozi wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini pamoja na wawakilishi wa mashirika ya kimataifa zilizofanyika Ikulu.

Aidha, Rais Samia amesema ili kuhakikisha uchaguzi huru na wa haki, Kikosi Kazi huru cha kupitia na kushauri mageuzi muhimu katika mfumo wa siasa kiliundwa ambapo kiliwasilisha ripoti yake mwaka 2023.



Rais Samia pia amesema mapendekezo mengi ya Kikosi Kazi yaliyopokelewa na serikali na wadau wote yalihusu kuongeza uwazi katika michakato ya uchaguzi ikiwa ni pamoja na uteuzi wa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi.

Vile vile, Rais Samia amesema masuala machache hayakupokelewa moja kwa moja ambayo yalikuwa kinyume na katiba hivyo yanaweza kuchukuliwa wakati wa mchakato wa marekebisho ya katiba.



Rais Samia amesema serikali itaendeleza ushirikiano na balozi hizo kwa mujibu wa katiba, tunu za kitaifa, usawa, umoja na mshikamano wa kitaifa huku akiwataka mabalozi hao kutokuingilia uchaguzi na kuzingatia mila, kanuni na maadili ya kidiplomasia.



Kwa upande mwingine, Rais Samia amesema Tanzania inasikitishwa na vita vinavyoendelea Palestina na kusababisha mauaji ya watoto na raia wasio na hatia na inaunga mkono usuluhishi kati ya Palestina na Israeli kwa kutoa wito wa kusitishwa mapigano na kupatiwa misaada ya kibinadamu.


Jumatano, 7 Februari 2024

Alcohol shortage hits Zanzibar Tourism Sector

 The spice islands of Zanzibar are facing a shortage of alcohol which threatens the tourism sector of one of Africa's top travel destinations.

Tourism generates about 90% of the Tanzanian archipelago's foreign revenue.

Prices of beer have shot up by almost 100% after the supply chain was disrupted by a sudden change of importers.




The islands' tourism minister resigned recently citing poor work conditions.

However, some have linked his resignation to the issues with alcohol supplies.

Known for their stunning sandy beaches and rich cultural heritage, the Indian Ocean islands are popular with tourists from around the world.

Last year, Zanzibar was ranked among the 10 best travel destinations in Africa by several tour magazines.

But hoteliers now warn that the problems over alcohol supply might make the island lose its tourism shine.

Several tourist hotels along the Matemwa beaches in the north of Zanzibar's main island are only serving soft drinks and people in that area say they have to go to the main city, Stone Town, for alcohol.

Mr Mshenga's business selling beer and sea food has been badly hit.

"We are running short of beer at my bar, and I just have a stock of soft drinks," he told the reporter. "The government has to take action. It is the high season now, it is very hot and these tourists need joy, they need cold beer on these beaches."




An American tourist, who did not want to be named, said: "I love Zanzibar and its beaches. The people are amazing and only challenge I feel now is I can't get hard liquor. I want to have spirits or even whisky but nothing is found in the hotel - they instead advised me to order it from Stone Town."

The local manufacture of alcohol is banned in Zanzibar, whose population is largely Muslim.


Most of the alcohol sold on the islands comes from mainland Tanzania, while some is imported from South Africa.

The initial shortage early this year began when the Zanzibar Liquor Control Board (ZLCB) delayed renewed permits for the three established importers - One Stop, Scotch Store, and ZMMI.

It is not clear why the licences of the three firms, which had supplied alcohol to the island for more than two decades, were not renewed.

For alcohol importers to get licensed, they must be Zanzibari-born residents with a clean tax record, a warehouse, and a delivery vehicle.

Additionally, importers must also pay a $12,000 (£10,000) annual fee to the regulatory board.




Last month, ZLCB granted licences to three new companies - Kifaru, Bevko and Zanzi Imports - but hoteliers say they are still struggling to meet the demand.

The new firms are reportedly entangled in a lengthy vetting process amid reports that some non-Zanzibaris are involved in the operations of the companies in contravention of the law.

The situation has been complicated further after the three previous licence holders filed appeals, asking the government to renew their liquor import permits.

Zanzibar's liquor stores are struggling to keep shelves stocked.


"There is an alcohol shortage in Zanzibar and we've already informed authorities about the tourism sector's situation," Rahim Mbarouk, chairman of the Zanzibar Tourism Investment Association, told the reporter.

The price of beer has gone up from 2,500 shillings ($1; £0.80) to 5,000 shillings, according to Neema Meena, a frequent traveller to Zanzibar from mainland Tanzania.

Some popular alcohol brands, like Safari, are said to be completely unavailable.

"This shortage hits hard," Frank John Kahamu, secretary at the Amani Alcohol Merchants Union, told privately-owned The Citizen website.

Mr Kahamu said more than 3,000 workers could lose their jobs if the situation continued.

"We can't keep paying wages with empty shelves."

ZLCB chairperson Juma Chum declined to respond when the reporter reached out for comment.

But Issa Mahfoudh Haji, a senior official in the Ministry of State responsible for the ZLCB, told state media: "We have heard about the complaints and we need to find details about the controversy."

Simai Mohammed Said resigned as tourism minister last week, citing "unfavourable and disruptive working conditions".

His resignation has been linked to a recent press conference where he publicly accused the ZLCB of mismanaging the liquor industry.

"If we fail to plan, including having enough stock of alcoholic beverages, we frustrate our visitors," he said, according to state media.

But while swearing in the new tourism minister on Thursday, Zanzibar President Hussein Mwinyi suggested Mr Said had a conflict of interest.

Reports link one of Mr Said's relatives to one company whose licence was not renewed.

"If you have a bar, and you find out authorities have not given access to alcohol to your bar, then be transparent and tell the public that there is conflict of interest," President Mwinyi said, referring to Mr Said.


The crisis comes amid soaring tourist arrivals in the semi-autonomous Tanzanian islands.

They witnessed a 16% surge in international visitors last year, welcoming a record more than 630,000 tourists, according to the annual tourism report.

The tourist upsurge was due to significant increases of arrivals from India and Russia, the report said.

Jumatano, 20 Novemba 2013

SHERIA ZA AJIRA KWA WATOTO (TANZANIA)

Ajira kwa Watoto

Je Sheria za kazi zinamuelezea vipi mtoto?
Kifungu cha 4 cha Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi ya mwaka, 2004 kinamuelezea mtoto kama mtu mwenye umri chini ya miaka 14 isipokuwa kwa ajira zilizo katika sekta hatarishi,  mtoto maana yake ni mtu mwenye umri wa chini ya miaka 18.
Je kuna sheria yeyote inayosimamia ajira kwa watoto?
Ndio, kuna sheria kadha wa kadha zinazoelezea ajira kwa watoto kama vile katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, sheria ya Watoto na sheria ya elimu na mafunzo ya ufundi stadi zikiwa ni miongoni mwa nyingi. Lakini linapokuja suala la ajira na kazi, Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2004 ndio inayokidhi hasa.
Je kuajiri mtoto inakubalika kisheria?
Kwa ufupi sheria inakataza mtoto mwenye umri chini ya miaka 14 kuajiriwa. Sheria pia inaendelea kukataza ajira kwa watoto chini ya miaka 18 katika maeneo ya migodi, viwanda, kama mabaharia katika meli au kazi nyingine yeyote inayotambulika kua hatarishi. Hata hivyo, sheria inaruhusu ajira kwa watoto wa miaka 14 katika kazi nyepesi ambazo sio hatarishi kwa afya ya watoto na maendeleo na haihatarishi mahudhurio ya watoto shuleni, ,mafunzoni au programu za kujifunza. Kwa ujumla ustawi wa watoto hautakiwi kuhatarishwa hata kidogo.
Je kuna adhabu kwa mtu atakayeajiri watoto kinyume cha Sheria ya Ajira na Mahusiano ya Kazi ya mwaka 2004?
Ni kosa kuajiri watoto kinyume na sheria ya kazi inavyosema na adhabu inatolewa chini ya kifungu cha 102 (2) ambacho kinampaHakimu wa Wilaya na Mkazi kutoa adhabu sawa na faini isiyozidi shilingi milioni 5 au kifungo cha mwaka mmoja au vyote faini na kifungo kama mahakama itavyoona inafaa, kutegemea na mazingira ya kesi yenyewe.

Ni vipi Waajiri watafahamu kua maeneo yao ya kazi ni hatarishi?
Sheria inamtaka Waziri kuandaa orodha ya sekta hatarishi na kuisambaza kwa umma. Kwa sasa kuna rasimu ya orodha hiyo kutoka kwa Waziri wa Kazi na Ajira lakini bado haijasambazwa na kua rasmi.
Je mwajiri atakua na makosa kwa kuajiri mtoto kwa kupewa taarifa zisizo sahihi au kutotambua?
Kama mwajiri atatoa madai kwamba hakufahamu kwamba mtu aliyemuajiri ni mtoto wakati wa kumpa ajira au kudai kupewa taarifa zisizo sahihi watakua na wajibu wa kuthibitisha kua ilikua sahihi kwa wao au mtu mwingine yeyote mwenye akili timamu kuamini kwamba mtoto huyo  alikua na umri wa kuajiriwa. Ni lazima waonyeshe kwamba kulikua na hatua za kutosha kuhakikisha hawaajiri watoto. Uthibitisho wa cheti cha kuzaliwa, kumbukumbu za usahili na wazazi wa mtoto na uthibitisho mwingine wowote kuonyesha kwamba walipotoshwa, hii itawasaidia kuwaepusha na adhabu iliyotajwa hapo juu.
Je mtu atakua na makosa kwa kukuwadia mtoto kwa ajira?
Sheria inakataza kuajiri mtoto na kukuwadia mtoto kwa ajira. Kama kutakua na uthibitisho kwamba kulikua na ukuwadi wa watoto kwa ajira basi mtu huyo atakua na makosa na atachukuliwa hatua sawa na Yule aliyeajiri mtoto au watoto katika maeneo yake ya kazi.